Latest Posts

WAGANGA WATAKIWA KUWAEPUKA WANASIASA WANAOWEZA KUWAWEKA MATATANI

Theophilida Felician, Kagera.

Katibu mkuu wa chama cha waganga TAMESOT Bw. Lukas Joseph Mlipu ametoa wito akiwataka waganga wa tiba asili nchini  kufanya kazi kwa umakini hususani kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu utakaofanyika mwezi Oktoba 2025.

Katibu huyo ameyabainisha  hayo wakati akiwahutubia waganga kwenye semina iliyofanyika kata ya Kibeta manispaa ya Bukoba mkoani Kagera ambapo amefafanua kuwa imezoeleka  nyakati kama hizi  waganga huwa kimbilio la wanasiasa kupata tiba kwa namna mbalimbali  hivyo ni wajibu wao kuwa chonjo kwani   yamekuwepo  mambo mengi yanayotendeka kwenye jamii mfano mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi Albino yakishatokea huwahusisha moja kwa moja waganga jambo ambalo siyo jema.

“Tuepuke uhalifu ndugu  zanguni  inatokea mtu anakatakata mtu huko anakimbilia kwako eti apate dawa asikamatwe   nawewe unapambana kwelikweli kumsaidia huo sini uhalifu?”sasa ukibainika unafanya hivyo wakukamate”amesema  katibu mkuu Lukas  Mlipu.

Hata hivyo akiwa mkufunzi wa mafunzo   yaliyolenga kuwanoa waganga  ili kuwajengea uwezo na weledi  amewasisitiza kuwa TAMESOT imejipanga kuinua sekta hiyo ambayo imekuwa ikizipitia changamoto kadhaa hasahasa kudharauliwa, kubezwa, kuonewa namengineyo huku akiwasihi kuwa wamoja nakukijenga chama hicho kwa  vitendo.

ACP Mpondera Rashidi ni mkuu wa polisi jamii mkoa Kagera kwaniaba ya kamanda wa polisi mkoa  amewaeleza kwamba baadhi ya  waganga wamekuwa wakihusishwa na ramuli chonganishi  na kufanya kazi bila leseni mambo ambayo ni kinyume na taratibu

Mpondera ameongeza kuwa kuelekea uchaguzi mkuu wa madiwani, wabunge na Rais TAMESOT haina budi kuwasimamia kikamilifu waganga wasihusishwe na  matukio ya namna yoyote   kinyume na leseni zao.

Yustas Nyakubaho ni mwenyekiti wa waganga wilaya Ngara akishukuru na kupongeza juhudi za katibu Mkuu Lukas Joseph Mlipu   amewakumbushia madhira waliyoyapitia kipindi cha wimbi la mauaji ya Albino hivyo ametoa wito akiwasihi wenzake wasiingizwe mitegoni na watu wasiokuwa na nia njema na taaluma hiyo

Latest Posts

Don't Miss

Stay in touch

To be updated with all the latest news, offers and special announcements.

error: Content is protected !!