Latest Posts

KITUO CHA MABASI, SOKO LA KISASA NA KINGO ZA MTO KUJENGWA BUKOBA

Theophilida Feliacin, Kagera.

Mbunge wa jimbo la Bukoba mjini Mhe Stephen Byabato ameipongeza na kuishukuru serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kukitatua kilio cha wananchi wa jimbo la Bukoba mjini baada ya kuanzisha ujenzi wa miradi mikubwa  mitatu yenye zaidi ya Sh  Bilioni 40.

Byabato ameyaeleza hayo akiwahutubia wananchi katika hafla fupi ya kuwakabidhi mikataba ya kuanza ujenzi wakandarasi shughuli iliyofanyika eneo la soko kuu la zamani  mjini Bukoba.

Ameitaja miradi hiyo ni pamoja na kituo kipya cha mabasi Kyakailabwa, soko kuu la kisasa na kingo za mto Kanoni miradi ambayo itakuwa yenye manufaa kwa wananchi wa Bukoba na mkoa kwa ujumla.

Amefafanua kwamba miradi hiyo nisehemu ya maombi aliyoayandika kwa  serikali  lengo  kuinua maendeleo ya Bukoba na baada ya taratibu kufanyika serikali imejibu  maombi hayo na miradi tayari inaanza ujenza ndoto ambayo niya muda mrefu kwa wakazi wa bukoba.

 

Amewashukuru viongozi wote walioungana naye katika kuihangaikia miradi hiyo bila kuwa sahau wananchi ambao wamekuwa naye bega kwa bega na matunda yamaendeleo yanaendelea kustawi kwa kasi  hivyo amewaomba kuendelea kuwa wamoja hususani kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu huku akisikitishwa  na hali ya siasa zenye viashiria vya chokochoko  zilizoanza kuchomoza  dhidi yake.

Mkuu wa mkoa Kagera Mhe Fatma Mwassa akiwa mgeni rasmi awali ameanza  kuishukuru serikali kwa miradi hiyo  ambapo amewataka wakandarasi kuijenga kwa wakati ndani ya muda wa miezi 15 kama yalivyo maelekezo ya mkataba.

Amewataka wananchi kuilinda miradi ili kuwawezesha wakandarasi kwenda kasi bila mkwamo kama yalivyo makundi ya serikali.

Latest Posts

Don't Miss

Stay in touch

To be updated with all the latest news, offers and special announcements.

error: Content is protected !!