Latest Posts

MAKUMI YA WATU WAFIKISHWA MAHAKAMANI KISA MAANDAMANO DHIDI YA UFISADI UGANDA

Makumi ya watu wamezuiliwa katika mji mkuu wa Uganda Kampala baada ya kujiunga na maandamano yaliyotawanyika ya kupinga ufisadi kupinga marufuku rasmi.

Kulingana na taarifa ya mawakili kutoka Uganda, takriban watu 60, akiwemo mtangazaji mashuhuri wa TV na viongozi watatu vijana wa maandamano, walifikishwa mahakamani kwa haraka na kurudishwa rumande kwa kushiriki maandamano ya kuelekea bunge la nchi hiyo siku ya Jumanne.

Rais Yoweri Museven, ambaye ameitawala Uganda kwa takriban miongo minne, alikuwa ameonya kabla ya tukio kwamba waandamanaji wanacheza na moto.

Maandamano hayo yaliandaliwa kwenye mitandao ya kijamii huku kukiwa na hasira kutokana na madai ya muda mrefu ya ufisadi yanayowahusisha maafisa kadhaa wa ngazi za juu wa umma, huku yakielezwa kuchochewa kwa kiasi kikubwa na maandamano ya mwezi uliopita nchini Kenya kwa sehemu, ambayo yalimlazimisha Rais William Ruto kusitisha nyongeza ya kodi iliyopangwa.

Hapo awali polisi walitangaza kuwa walikataa kutoa kibali cha kuandamana na hawataruhusu maandamano yoyote ambayo yanatishia amani na usalama wa Uganda.

Msemaji wa polisi Kituuma Rusoke alisema mamlaka haitaruhusu maandamano yoyote ambayo yanatishia “amani na usalama” wa Uganda.

Ufisadi unaelezwa kuwa ni tatizo kubwa nchini Uganda huku kukiwa na kashfa kadhaa za hali ya juu zinazohusisha maafisa wa umma, na nchi hiyo imeorodheshwa katika nafasi ya chini 141 kati ya nchi 180 kwenye ripoti ya ufisadi ya Transparency International.

Latest Posts

Don't Miss

Stay in touch

To be updated with all the latest news, offers and special announcements.

error: Content is protected !!