Latest Posts

BABU AJINYONGA BAADA YA KUMBAKA MJUKUU, AACHA UJUMBE MZITO KWA FAMILIA

Kijiji cha Kifuni kilikumbwa na mkanganyiko wa hisia juu tukio lililomuhusisha Wenseslaus Ulomi, mzee wa miaka 50 aliyekutwa amejinyonga nyumbani kwake, Septemba 2, 2024.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro Simon Maigwa, Wenseslaus alijinyonga kwa kutumia shuka ndani ya chumba chake baada ya kufahamu kuwa mkewe Philipina Olomi amegundua kuwa alimfanyia ukatili huo mjukuu wao, aliyekuwa akisoma darasa la kwanza katika kijiji hicho.

Kwa mujibu wa taarifa iliyochapishwa katika tovuti ya Mwananchi, siku ya tukio Ulomi alirudi nyumbani akiwa amelewa na kumfukuza mkewe, jambo ambalo Philipina alithibitisha katika mahojiano.

“Nikamwambia kwa nini unataka unifukuze, akaniambia nataka uondoke hapa nyumbani kwangu, nikamwambia wewe mbona kila siku huku nyumbani ni ugomvi mbona hupumziki na ninaumwa? akaniambia toka tu ili nipate amani, ukiwa hapa sina amani kabisa,” anaeleza mama huyo.

Philipina aligundua ukatili huo baadaye baada ya kumchunguza mjukuu wake, jambo ambalo lilimshtua sana. Katika hali ya kuchanganyikiwa, aliamua kumshirikisha mama mkwe wake na kumweleza kuhusu tukio hilo. Mama mkwe alishauri kuondoa mtoto shule na kumtafuta shangazi yake ili kushauriana zaidi.

Wenseslaus alipojua kuwa mkewe amejua ukweli, aliandika ujumbe wa mwisho, akiwataka mke wake na watoto wao sita kutoshiriki katika mazishi yake.

Mtoto huyo wa miaka minane, ambaye jina lake limehifadhiwa, aliweza kuelezea kilichomkuta kwa uchungu.

“Babu alinichukua, akanipeleka kitandani kwake, akanifanyia vile, kisha akanipa Sh400 na kuniambia nisimwambie mtu,” alisema mtoto huyo kwa huzuni.

Mwili wa Wenseslaus Ulomi unatarajiwa kuzikwa Septemba 7, 2024, huku familia ikiwa imegawanyika kutokana na maamuzi ya marehemu kuacha ujumbe huo wa mwisho unaowataka mkewe na watoto wake kutoshiriki mazishini. Tukio hili limeacha kijiji kikiwa na maswali mengi juu ya hatma ya familia na pia athari za ukatili wa kijinsia, hasa kwa watoto.

Latest Posts

Don't Miss

Stay in touch

To be updated with all the latest news, offers and special announcements.

error: Content is protected !!