Baada ya shahidi P8 kumaliza kutoa ushahidi wake Lissu alipewa nafasi ya kuuliza maswali ya dodoso(cross examination)
Lissu: Ukionyeshwa maelezo yako uliyoandika utayatambua
Shahidi: Sio jukumu langu ni la mawakili
Lissu: Unabishana na Mwenyekiti wako?
Shahidi: Sasa hivi wewe si Mwenyekiti ni mshtakiwa.
Lissu: Umesema 22/04/2025 ulipoenda kuripoti kwa RCO ulichukuliwa na afande akakupeleka kwenye ofisi ya afande mwingine Michael tuonyeshe kama kuna sehemu umeandika hayo.
Shahidi: hakuna sehemu kama hiyo
Lissu: Haya yote nimekuuliza na hayapo kwenye maelezo uliyoandika umesema mahakamani kwa sababu unaamini yana maanakweli au si kweli.
Shahidi: kweli
Lissu: Nitakosea nikisema kwamba hukusema polisi kwa sababu unaamini sio mambo muhimu
Shahidi: Utakosea
Lissu: Waeleze majaji kama umeeleza kwa nini hayo mambo hukuyasema 22/4/2025
Shahidi: Hapana
Lissu: Umesema Mwenyekiti alisema tutakinukisha Waeleze majaji kama katika hayo uliyoyasikia akisema tutakinukisha alieleza maana ya tutakinukisha
Shahidi: Uliieleza
Lissu: Nilisema ni nini
Shahidi: Kukinukisha ni kama tunafanya uasi
Lissu: Unafahamu maana ya kukinukisha kwa kiswahili
Shahidi: Ni hivo kukinukisha
Lissu: Inatokana na neno nuka au nukia
Shahidi: Mi nafahamu neno kukinukisha hayo mengine mi sielewi
Lissu: Waeleze majaji kama hiyo video uliyoiona mtandaoni umewasilisha leo mahakamani
Shahidi: Hapana
Lissu: Hasira zako ni kwa sababu ya wizi wa uchaguzi
Shahidi: Hayo najua moyoni mwangu twende kwenye point
Lissu: Waeleze majaji kama kuanzia tarehe 4/4/2025 Lissu ametoa kauli
Shahidi: Hajatoa kwa sababu ni mhalifu
Lissu: Ngoja nukuweke sawa kwa sababu we ni mwanachama wangu huwezi ukanisumbua
Shahidi: Mimi sio mwanachama wako mshtakiwa
Lissu: Umenigeuka
Shahidi: Kwa sababu umeniingiza kwenye hatia sikutarajia hata siku moja nitakuja sehemu kama hii.
Lissu: Waeleze majaji tangu ulivyoandika maelezo haya 2025 uliwasiliana na Polisi mara ngapi
Shahidi: Juzi tarehe 14 nilipigiwa simu nikiwa nyumbani natakiwa kufika Dar es Salaam
Lissu: Waeleze majaji kama umetishiwa na Kiongozi wa CHADEMA, mwanachama mfuasi
Shahidi: Nakumbuka alisema mtu yeyote anaetoa ushahidi kwa Mwenyekiti wetu lazima tusalimiane nae
Lissu: Aliyekuwa anasema hayo maneno ni nani
Shahidi: Ni watu ni mwanaume haiwezekani kumtaja kwa ajili ya ulinzi wangu binafsi.
Lissu: Kuna kiongozi yeyote wa CHADEMA au mfuasi alietishia ndugu zako
Shahidi: Hakuna maana hawanijui
Lissu: Umesema ulivyokamatwa tarehe 8/4/2025 ulihojiwa Polisi
Shahidi: Sikuhijiwa polisi nilihojiwa kwenye ofisi ya RCO
Lissu: Huyu RCO ni Polisi au Bwanamifugo
Shahidi: Mbona una maswali ya kitoto aise
Lissu: Nitakosea kwamba nikisema umefutiwa kesi ili uwe shahidi kwenye kwsi hii
Shahidi: serikali achana nayo sikutegemea, niliongea ukweli na leo nimejikuta huku.
Baada ya maswali ya dodoso kuisha hapakuwa na maswali ya Re-examination kutoka kwa jamhuri hivyo waliomba shauri kuahirishwa kwani hapakuwa na shahidi mwingine aliyeandaliwa kwa leo.
Ombi hili lilikubaliwa japo Lissu alipinga akitaka Jamhuri waamrishwe na kuleta mahakamani shahidi ambaye yupo hapa jijini Dar es Salaam jambo. Jaji Dunstan Ndunguru alitoa amri kwa Jamhuri kuanzia kesho kuleta mashahidi kuanzia watatu na kuendelea.