Latest Posts

KIJANA WA MIAKA 26 AHUKUMIWA KUNYONGWA KWA MAUAJI YA WA WATU WATATU KATAVI

Mahakama Kuu ya Mkoa wa Katavi imemuhukumu Shija Charles (26), Kunyongwa hadi kufa baada ya kupatikana na hatia katika kesi ya mauaji ya kukusudia ya watu watatu wa familia moja huko katika kitongoji cha Busongola,kata ya Bulamata, Wilaya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi.

Akisoma hukumu hiyo, Hakimu Mfawidhi Sumary Gway amesema mshitakiwa alitenda kosa hilo Februari 5, 2024 ambapo  aliwaua Monica Kingwa (24), Siwema Shija (2) na Yanga Shija mwenye umri wa miezi 8 kwa kuwashambulia kwa kitu chenye ncha kali (panga )sehemu mbalimbali za miili yao, tukio linalodaiwa kuhusishwa na imani za kishirikina za kutafuta utajiri.

Aidha Gway amesema mshitakiwa huyo alitenda kosa hilo kinyume na kifungu cha 196 cha kanuni ya adhabu sura ya 16 iliyofanyiwa marejeo mwaka 2022 na kueleza adhabu hiyo imetolewa ili iwe fundisho kwa washitakiwa na jamii katika kukomesha vitendo vya kikatili.

Awali Kesi hiyo ilifikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza Juni 14, 2024 na hukumu kutolewa Machi 23, 2026  ambapo Hakimu Mfawidhi amebainisha kuwa mahakama imejiridhisha pasiposhaka na ushahidi uliotolewa na upande wa Jamhuri na umetosha kumtia hatiani mtuhumiwa.

Latest Posts

Don't Miss

Stay in touch

To be updated with all the latest news, offers and special announcements.

error: Content is protected !!