Latest Posts

NSUMBA SEKONDARI WALIA CHANGAMOTO YA MAJI

Wanafunzi na walimu wa shule ya Sekondari Nsumba iliyopo katika Kata ya Luchelele Jijini Mwanza wameiomba Serikali kuwapelekea huduma ya maji ya uhakika ili kuwaondolea usumbufu wanafunzi kutafuta huduma hiyo sambamba na kuondoa hatari ya kupata magonjwa ya mripuko kama kipindupindu.

Wakizungumza leo kwenye mahafali ya 27 ya kidato cha sita shuleni hapo, Mkuu wa shule hiyo, Denis Mwakisimba amesema kwa sasa shule hiyo inapata huduma ya maji angalau mara moja kwa wiki hali ambayo ni hatari kwa wanafunzi kutokana na kuwa na mahitaji makubwa ya maji hasa kwenye uendeshaji wa mifumo ya maji taka.

Hata hivyo ameongeza kuwa kutokana na ukubwa wa tatizo hilo kwa hatua ya dharula wanaomba wapate matenki ya lita 5000 ya kuhifadhia maji sambamba na kuchimbiwa kisima cha maji.

“Tunayochangamoto kubwa sana upatikanaji wa huduma ya maji kwa kweli wanafunzi wanapata shida sana kwenye eneo hili ukizingatia miundombinu yote inategemea maji, saizi walau tunapata maji mara moja kwa wiki wakati huo nina vijana karibu 1000 na uendeshaji karibu wote wa mifumo ya majitaka unategemea maji,” amesema Mwakisimba

Akisoma Risala kwa niaba ya wahitimu wenzake, Daudi Magwega mbali na kuitaja changamoto hiyo pia wanafunzi hao wameiomba Serikali wapate gari kwa ajili ya usafiri sambamba na kujengewa uzio wa shule ili kupunguza matukio ya wizi na matamanio kwa mabinti wanaokatiza shuleni hapo.

Mgeni rasmi ambaye ni Naibu Meya Jiji la Mwanza, Anitha Lwezahula ameahidi kuwatatulia changamoto hiyo ya maji shuleni hapo ambapo kwa kuanzia ametoa Milioni moja kwa ajili ya kununua matenki ya kuhifadhia maji.

 

Latest Posts

Don't Miss

Stay in touch

To be updated with all the latest news, offers and special announcements.

error: Content is protected !!