Latest Posts

KESI YA VIGOGO CHADEMA KUKIUKA AMRI YA MAHAKAMA KUSIKILIZWA OKTOBA 22

Kesi ya jinai namba 25480 ya mwaka 2025 iliyofunguliwa kwenye Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala ndogo ya Dar es Salaam na aliyewahi kuwa Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Zanzibar Said Issa Mohamed na wenzake wawili (Ahmed Rashid Khamis na Maulidah Anna Komu) dhidi ya viongozi waandamizi wa chama hicho wakiongozwa na Makamu Mwenyekiti wake wa Tanzania Bara John Heche imetajwa leo Mahakamani hapo chini ya Jaji Awamu Mbagwa

Katika kesi hiyo, vigogo hao wa CHADEMA wanatuhumiwa kukiuka amri ya Mahakama Kuu iliyotolewa Juni 10.2025, kufuatia uwepo wa kesi ya madai inayohusu usawa kwenye mgawanyo wa mali ndani ya CHADEMA inayosikilizwa chini ya Jaji Hamidu Mwanga, ambapo wadaiwa wamepigwa marufuku kujihusisha na shughuli zozote za kisiasa na matumizi ya raslimali za chama hadi hapo kesi hiyo itakapotolewa uamuzi

Leo Mahakamani hapo, upande wa mashtaka umewasilishwa flash ambayo ina picha jongefu (video) zinazoonesha kauli zilizotolewa kwa nyakati tofauti kupitia majukwaa tofauti, kauli ambazo zinadaiwa kukiuka amri ya Mahakama ya Juni 10.2025

Hata hivyo, kesi hiyo imepangwa kusikilizwa Oktoba 22.2025 saa 05:00 asubuhi kutokana na kile kilichoelezwa na Mahakama kuwa imefunguliwa kwa hati ya dharura, pia waleta maombi wametakiwa haraka iwezekanavyo kuwapatia taarifa baadhi ya watuhumiwa ambao hawajawafikishia taarifa hiyo

Wakati huohuo, upande wa utetezi umetakiwa kuwasilisha kiapo kinzani hadi kufikia Oktoba 21.2025

Hadi kufikia leo ni washtakiwa watatu (3) pekee ndio waliokuwa wamepatiwa taarifa za uwepo wa kesi hiyo ambao ni John Mnyika, Bodi ya Wadhamini na Katibu Mkuu wa CHADEMA, ambapo wahusika wamefika Mahakamani sambamba na Mawakili wao Mpale Mpoki na Hekima Mwasipu

Washtakiwa ambao hadi leo walikuwa hawajapata taarifa hiyo na hivyo Mahakama kuagiza wapatiwe kwa haraka ni pamoja na John Heche, Rose Mayemba, Brenda Rupia, Hilda Newton, Twaha Mwaipaya na Gervas Lyenda

Katika kesi hiyo, upande wa mashtaka umewasilishwa na Mawakili wawili (2) ambao ni Shaban Marijani na Alvan Fidelis.

Latest Posts

Don't Miss

Stay in touch

To be updated with all the latest news, offers and special announcements.

error: Content is protected !!