Na Helena Magabe- Tarime
Mwenyekiti wa chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA) Wilaya ya Tarime ambanye pia amewahi kuwa Makamu mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Tarime Mhe Bashiri Abdalla Suleiman(Sauti) amewataka Madiwani kupitia Halmashauri pamoja na Mbunge Mhe Michael Kembaki na wote wanahusika kuweka bei rafiki ya vibanda vya sokokuu kwani bei hiyo haijapangwa na Serikali kuu bali imepangangwa na Madiwani ambapo kesho mei 19 maombi yananza kutumwa.
Akizungumza na Waandishi wa habari Mei 18,2025 amesema bei ya vibanda na vizimba iyopangwa na Halmashauri sio rafiki kwa wananchi ni kubwa mno hivyo amewaomba Madiwani pamoja na Mbunge kukaa na kupanga upya bei hizo kwa kuzingatia hali ya Wananchi vilevile mfumo unatumika kuomba maombi wa kidigitali (TAUSI) nao amesema sio rafiki kwani sio watu wote wanaoweza kutumia simu janja na kwamba haamini wataohitaji vizimba 144 kuwa wote Wana simu jaja hivyo ni vema utumike utaratibu uliozoeleka wa kuandika maombi .

Amesema kwa mujibu wa Watumishi wa Halmashauri soko lina vibanda 321 na vizimba 144 bei zimeanishwa vibanda vinavyotazamana na eneo la stendi kuu ambavyo viko double bei yake ni 300,000 kila kibanda,vibanda vilivyo ndani ambavyo ni double 260,000,Vibanda vya chini single 150,000,vibanda vya nje juu single 130,000,vibanda vya ndani single 130,000 pamoja na kila kizimba 15,000 ambavyo pia ameomba bei yake iangaliwe upya ,au watalamu wasajili wao kisha watoze kila kizimba 20,000.
Suleimani amesema kwa mujibu wa Ibara ya 8 kifungu kidogo cha kwanza “A” hadi “D “ni wazi kwamba Madiwani na Mbunge wameshindwa kuwatetea Wananchi kwa viwango vikubwa hivyo vya kodi na kwa kizingatia kuwa Ibara hiyo ndiyo imewaweka madarakani kwa kupitia Wananchi kwani ni vema wakaweka viwango rafiki ili iwe rahisi kulipia.
Amefafanua kuwa kipindi akiwa Makamu mwenyekiti wa Halmashauri 2015-2020 walijenga vibanda uwanja wa mpira ambavyo walivipangisha kwa shilingi 50,000 kwa mwezi katika kodi hiyo 30,000 kwaajili ya mmiliki wa kibanda na 20,000 kwaajili ya Halmashauri kodi ambayo inaendelee hadi leo na ni kodi ambayo haimuumizi Mwananchi.
Amezungumzia pia kigezo cha kuwa na reseni ndio mtu apewe kibanda amesema si sahihi kwani inawezekana mtu ndio anaanza biashara anahitaji kibanda hivyo kwa kigezo hicho atakosa ameshauri waige mfano TRA ambao mtu anapoanza biashara wanamtembelea na kumkadilia kulingana na biashara yake.
Jitihada za kumpata Mwenyekiti wa Halmashauri hazikufanikiwa lakini Diwani mmoja jina limehifafhiwa alisema kabla ya Baraza la Madiwani kupitisha kikao cha CMT ndicho kinakaa na kujadili kwanza kisha Baraza kupitisha lakini pia amesema soko lilijengwa kwa pesa za TAMISEMI bei zilizoainishwa hapo ziliwekwa ili kupokea maoni kwa wananchi zimeshushwa juu mapendekezo yamekuwa 100,000 na chini 130,000 kesho zitatitumwa na Mkurugenzi TAMISEMI majibu kamili ni jumanne.
Hata hivyo tayari Wananchi tangu juzi walikuwa na manung’uniko juu ya kodi hizo wakidai kuwa kodi ni kubwa na vibanda ni vidogo vifinyu pia ukilinganisha na vimbanda vya uwanja wa mpira ambavyo vina bei nafuu lakini ni vikubwa ikumbukwe tu kuwa mladi huu wa soko pia ulianzishwa enzi Halmashauri ikiongozwa na CHADEMA chini ya mwenyekitibwa Halmashauri 2015-2020 andiko la mladi liliandikwa na Mhe Easther Matiko akiwa Mbunge wa Jimbo la Tarime Mjini.
Kwa upande mwingingine amezingumzia hali tete ya ulinzi na usalama katika Mji wa Tarime kufatia matukio mbali mbali ya kiharifu yanayoendelea yakiwemo matukio ya Kata ya Turwa mfano la Mama kuuwawa jana mkazi wa kata hiyo amemwomba Mkuu wa Wilaya Meja Edward Gowele ambaye ni mwenyekiti wa kanmati ya ulinzi na usalama ya Wilaya kushirikiana na Jeshi la polisi kupitia OCD kamati yake yote ya ulinzi na usalama vile vile washirikiana na WDC kudhibiti matukio hayo kwani hali ya usalama ni mbaya.