Latest Posts

MWILI WA ALIYEKUWA M/KITI HALMASHAURI YA NZEGA MJI WAZIKWA

Mkuu wa mkoa wa Tabora Paulo Chacha ameongoza mamia ya waombolezaji katika mazishi ya aliyekuwa Diwani wa Kata ya Itilo na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Nzega Mji wilayani Nzega mkoani Tabora kupitia Chama cha Mapinduzi CCM  Paschal Kigalu   yamefanyika leo February 19,2026 Wilayani humo.

Paschal kigalu alifariki dunia usiku wa kuamkia Februari 17,2026 kufuatia ajali ya barabarani ambayo imehusisha gari alilokua amepanda kugongana na gari jingine wakati alipokuwa kwenye mizunguko yake binafsi.

Akizungumza na waombolezaji Rc Chacha mbali na kutoa pole amewataka kuwa wavumilivu kwa kipindi hiki kigumu  pamoja na kuwasisitiza kuyaenzi yale mazuri  aliyokua akiyafanya  marehemu katika jamii , Kata na  halmashauri  kwa ujumla  kwa mustakabali wa maendeleo ya eneo hilo.

 

Latest Posts

Don't Miss

Stay in touch

To be updated with all the latest news, offers and special announcements.

error: Content is protected !!