Latest Posts

PPA YAWAASA VIJANA KUTOKUBALI KUTUMIKA KUIVUNJA AMANI

Theophilida Felician Kagera.

 

Vijana mkoani Kagera na Tanzania kwa ujumla wametakiwa kuwa makini nakuwaepuka watu wanaoweza kuwashawishi ili kushiriki matendo ya vurugu zenye kuihatarisha amani ya nchi hususani kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu wa  Oktoba.

Wito huo umetolewa na viongozi wa taasisi ya mabalozi wa amani Tanzania PPA  yenye makao yake manispaa ya Bukoba.

Viongozi hao wakizungumza na vyombo vya habari wamefafanua kwamba nyakati kama hizi kundi la vijana huonwa kama kundi muhimu hivyo hujikuta wakitumiwa na watu mbalimbali wakiwemo wanasiasa kwa malengo yakuwavusha katika harakati zao za kisiasa na wengine huwatumia ndivyosivyo hali inayopelekea kuwepo kwa matukio yavurugu hadi uvunjifu wa amani.

Maulid Rashidi Kambuga ni mkurugenzi wa taasisi amesema amani ikishatoweka hakuna pakukimbilia iwe kwa  vijana, wazee, akina mama, watoto wote wanaathirika.

Naye Mchungaji  Clavery Venant ambaye ni mkurugenzi msaidizi wa PPA amebainisha kuwa kundi la vijana hawanabudi kuishi kwa hofu ya Mungu na kuzingatia misingi ya maadili mema.

Bahati Ildephonce ni mkazi wa Bukoba yeye ameeleza  kuwa amani ikishavunjika husababisha madhara mengi kwa jamii hasa maumivu, vifo, kuteteleka kwa uchumi na miundo mbinu.

Kwa pamoja wametoa wito kwa wananchi kuwa wazalendo wa kweli ili kuilinda nakujenga Tanzania ya amani  kwani Tanzania ni moja tuu ikishaponyoka  hakuna kimbilio.

Latest Posts

Don't Miss

Stay in touch

To be updated with all the latest news, offers and special announcements.

error: Content is protected !!