Latest Posts

TARURA MOROGORO WATAKIWA KUKAMILISHA UJENZI WA DARAJA LA LUKUYU

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa TAMISEMI (Miundombinu) Mhandisi Rogatus Mativila ameagiza TARURA Morogoro kuhakikisha wanakamilisha ujenzi  wa  daraja la Lukuyu lililopo Kata ya Bigwa Manispaa ya Morogoro ifikapo Agosti 2024 ili kuwaondolea adha wananchi wa maeneo hayo kusafirisha mazao ikiwamo ndizi na kubeba mbogamboga kichwani.Mativila ameyasema hayo Juni 19, 2024 wakati akifanya ziara ya ukaguzi wa miundombinu ya barabara  mkoani humo ambapo amesisitiza kuwa ni wakati sasa wananchi kuondokana na changamoto ambayo imekuwa ikiwakabili kwa muda mrefu.

Daraja la Lukuyu limegharimu kiasi cha Shilingi milioni 70 linaenda kuwa mwarobaini kwa wakazi wa kata ya Bigwa Manispaa ya Morogoro.

Latest Posts

Don't Miss

Stay in touch

To be updated with all the latest news, offers and special announcements.

error: Content is protected !!