Latest Posts

UBADHIRIFU WA FEDHA ZA TASAF WAMCHEFUA ADO SHAIBU, AITAKA SERIKALI KUFANYA UCHUNGUZI

Katibu Mkuu wa ACT Wazalendo Ado Shaibu amesikitishwa na watu wanaofanya ubadhirifu wa fedha za  mpango wa kunusuru kaya maskini  (TASAF) maeneo mbalimbali hapa nchini

Ado ametoa kauli hiyo Agosti 07.2024 wakati akiwahutubia wakazi wa Manispaa ya Bukoba, mkoani Kagera katika maeneo ya kata ya Rwamishenye ambapo amesema kuwa ipo changamoto kubwa ya ubadhirifu  wa fedha hizo za wanufaika wa mpango huo ambao unawelenga wananchi maskini

Ameeleza kwamba tatizo hilo amelikuta maeneo mengi kwenye mikoa aliyopita katika ziara yake hivyo ameshangazwa kuona na Bukoba pia linajitokeza baada kupokea taarifa ya viongozi wa ACT Wazalendo ngazi ya mkoa na jimbo

“Kuna ubabaishaji mkubwa sana kwenye miradi ya TASAF na sisi tumemwambia Rais Samia nikiwa Mwanza na narudia tena kama hatoingilia kati na kuchunguza kwa umakini mkubwa mpango wa serikali wa kuzikwamua kaya maskini unakwenda nje ya mstari, kila tunakopita tumekuta ubabaishaji mkubwa sana  matatizo yake makubwa  ni matatu kwanza waratibu wa TASAF wanafanya ubadhirifu na upendeleo mkubwa,  wanaweka majina ya watu wasiostahili, maeneo mengine tumekuta wanaweka mpaka majina ya marehemu lakini wanaostahili hawapati fedha wasiostahili ndo  wanapata  wakati mwingine kwa kufuata ukada ndio wanapewa  fedha hizo” -Addo

Aidha, ameitaja changamoto nyingine kuhusiana na TASAF ni pamoja na utaratibu wa kuanzisha miradi ikiwemo ya ujenzi wa Barabara kutokana na mpango huo jambo alilolidai kuwa halifai kuendelea kufanyika

Katibu Mkuu huyo pia amezungumzia changamoto ya ukosefu wa kituo cha uhakika cha mabasi kwa muda mrefu mjini Bukoba akisema kwamba licha ya ahadi za muda mrefu kutoka kwa viongozi mbalimbali wa serikali na CCM bado hali imeendelea kuwa ileile  ya kukosekana kwa kituo hicho, hiyo ikiwa ni sambamba na  changamoto ya matibabu bure kwa watoto wa umri  wa mwezi 0 hadi miaka mitano pamoja na akina mama wajawazito

Hata hivyo suala la hali ya umaskini kwa mkoa wa Kagera hakusita kulielezea  kwa kuwa kiwango cha pato kiko chini ukilinganisha na takwimu ambazo zimekuwa zikitolewa mara kwa mara na Benki Kuu ya Tanzania

Amedai kuwa Kagera ni mkoa uliokaliwa lasirimali za kutosha hivyo haupaswi kuendelea kuwa kwenye orodha ya mikoa inayoshika nafasi ya mwisho kwa umakini, amewahakikishia wananchi  kuwa chama hicho kimejipanga vilivyo kusimama imara katika kuyashughulikia yale yote yanayoenda kinyume kwa wananchi

Katika hatua nyingine amekemea vikali  kitendo cha kuwatumia makada wa chama cha mapinduzi (CCM) kuhusika na zoezi la kuandikisha daftari la wapiga kura linaloendelea  akiweka wazi kuwa kufanya hivyo ni kinyume cha sheria jambo ambalo halivumiliki

Katibu Mkuu huyo ambaye katika mikutano yake anafanya zoezi la kuwasajili wanachama anaendelea na ziara yake ya siku nne mkoani Kagera

Nao viongozi wa chama ngazi ya jimbo na mkoa akiwemo Mwenyekiti wa mkoa wa Kagera Evodiu Justinian amezitaja kero kadhaa ikiwemo ya changamoto zinazojitokeza kwenye vituo vya kuandisha daftari la wapiga kura hasa ugomvi wa makada wa vyama vya siasa  CCM na CHADEMA wakiwabagua baadhi ya watu kutokuandikishwa, kodi kubwa kwa wafanyabishara wadogo, wingi  wa vizuizi Barabarani na  zaidi ubadhirifu wa  miradi ya TASAF

Viongozi hao wametoa angalizo kwa Mkuu wa Polisi wilaya ya  Bukoba  kutokufumbia macho ‘chokochoko’ hizo kwani zinaweza kuleta uvunjivu wa amani kama hazitodhibitiwa.

Latest Posts

Don't Miss

Stay in touch

To be updated with all the latest news, offers and special announcements.

error: Content is protected !!