Latest Posts

UVCCM YAIOMBA SERIKALI KUUFUNGIA MTANDAO WA X (TWITTER)

Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) waimeitaka serikali kupitia Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kuhakikisha inaufungia mtandao wa ‘X’ zamani ukijulikana kama Twitter kwa kudai kuwa mtandao huo unatangaza dhamira ya kuruhusu kupokea maudhui yanayokinzana  na mila, desturi na silka ya Watanzania.

Hayo yamezungumzwa na Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Mohamed Ali Mohamed Kawaida wakati akizungumza na wanahabari Jumanne Juni 11, 2024 jijini Dar es Salaam ambapo amesema hatua ya kuufuta mtandao huo itasaidia kuendelea kulinda maadili ya vijana wa Tanzania kwa kuwa  mitandao ya kijamii haipaswi kupewa kipaumbele kama inachochea uvunjifu wa mila na desturi.

Kawaida amesema hivi karibuni mtandao huo X umetoa tangazo ukieleza kwamba maudhui yote ya kingono na yale yanayofanana na hayo yameruhusiwa kupokelewa jambo ambalo halikubaliki kwenye taswira ya jamii ya Tanzania.

Amesema taarifa hiyo ya kusikitisha imepokelewa kwa hisia hasi na UVCCM hivyo kuitaka serikali kuchukua maamuzi kama iliyowahi kuchukua siku za nyuma ambapo serikali ilifungia mitandao iliyokuwa ikipandisha maudhui kama hayo.

Latest Posts

Don't Miss

Stay in touch

To be updated with all the latest news, offers and special announcements.

error: Content is protected !!