Mashuhuda wanasema kwamba kelele za maumivu kutoka chumbani ziliwashtua wahudumu wa hoteli, ambao walipojaribu kuingia ndani walikuta mlango umefungwa kwa ndani. Ilibidi wavunje mlango, ndipo wakawakuta wawili hao wakiwa wamelala uchi na wakilia kwa uchungu, wakiwa wamekamatana na kushindwa kutengana hata walipojaribu kujitoa kwa nguvu.

“Hatukuamini macho yetu. Tulipoingia chumbani, walikuwa wakilia kwa sauti huku wakiomba msaada. Ilikuwa hali ya kuogofya na ya ajabu sana,” alisema mmoja wa wahudumu.
Wito ulipelekwa kwa maafisa wa usalama, lakini badala ya kuwapeleka hospitali moja kwa moja, mwenye hoteli alishauri wawasiliane na mganga mmoja wa kienyeji ambaye anaaminika kusaidia kwenye visa vya aina hiyo. Soma zaidi hapa.