Latest Posts

MASWI AWA GUMZO KWA KUTHAMINI WAANDISHI WA HABARI MARA

Na Helena Magabe, Mara.

‎Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Eliakimu Chacha Maswi amekuwa mfano wa kwanza wa kuingwa na viongozi wengine pamoja na jamii kwa kuwa kiongozi wa kwanza wa serikali, kujali na kuthamini waandishi wa habari mkoani kwake Mara kwa kuwanunulia kompyuta mpakato za kisasa kwaajili ya kurahisisha utendaji kazi wao ambapo amekuwa gumzo na kivutio kwa waandishi Mara.

‎Maswi ambaye ni mdau mkubwa wa sekta ya habari na maendeleo kwa ujumla ameoyesha kujali, kusikiliza na kuthamani waandishi wa habari mkoani kwake kwa kuwanunulia waandishi wa habari 14 kompyuta mpakato (laptop) za kisasa zenye thamani ya zaidi ya milioni kumi na moja 11.4 kwaajili ya kurahisisha utendaji kazi wao kulingana na ukuaji wa teknolojia ya sasa.

‎

‎Hatua hii imekuja kutokana na waandishi kuomba pindi walipokutana naye nyumbani kwake Magoto Wilayani Tarime mwishoni mwa mwezi Juni wakitaka kufahamiana naye na kutaka kujua kama atatia nia kugombea ubunge kulingana na minong’ono iliyokuwa ikisikika kwa wananchi, na hapo ndipo mmoja alitoa ombi kwa kiongozi huyo likapokelewa na hatimaye likafanyiwa kazi na kutekelezwa.

‎Mwandishi aliyetoa ombi hilo ni Agustine Mgendi wa Azam Tv Mara. nakumbuka aliwasilisha ombi lake kwa kusema hivi, ” waandishi tuna uhaba wa vitendea kazi, mwandishi naye ni binadamu na yeye ana uhitaji” Maswi akashangaa kidogo kusikia baadhi ya waandishi hawana kompyuta, wengine hawana kamera na wengine hawana vyote kwa pamoja lakini alipokea ombi na kuahidi kulifanyia kazi.

‎Hatimaye sasa amewafanya waandishi kuwa wa kisasa zaidi kwa kuwanunulia kompyuta za kisasa zitakazorahisisha utendaji kazi wao katika mazingira yoyote bila shida , hii imekuwa ni heshima kwa tasnia hii ambayo jamii ilikuwa ikiitazama kama kundi lisilo na uhitaji licha kuwa hii ni tasnia  yenye changamoto kubwa na vitendea kazi vyake ni vya ghalama kubwa vinavyohitaji uwezeshwaji toka kwa wadau mbalimbali wa maendeleo.

‎Waandishi ambao ni nguzo maendeleo endelevu wanastahili kuungwa mkono kwa vitendo, hatua hii ya Maswi ni matumaini yetu waandishi wa Mara kuwa itakuwa chachu ya kufungua milango kwa wadau wengine wa Habari ikiwemo viongozi wa serikali na wa sekta binafsi, mashirika mbali mbali na kampuni kubwa za uwekezaji zilizopo nchini kuangalia wanachoweza kuwawezesha waandishi.

 

‎Waandishi walionufaika na kompyuta hizo wamepongeza hatua hiyo na kumshukuru kiongozi huyo kwa uzalendo wa kuthamini mchango wao wa habari kwa kuonyesha upendo wa hali juu, kwa katumia pesa yake kwa maslahi mapana ya wengi kwani kompyuta hizo zitatumika kwa maendeleo endelevu ya jamii yote, huku wakimwomba asikomee hapo aendelee kuwasaidia ili kuboresha mazingira yao ya kazi.

‎Aidha ikumbukwe kuwa yupo kiongozi mwingine ambaye aliwahi kuthimini waandishi kwa kuwanunulia kamera Waandishi wa habari wote wilayani Tarime huyu alikuwa Mbunge wa Jimbo la Tarime 2010-2015, alikuwa anaitwa   Nyambari Nyangwine ambaye kwa sasa ni mtia nia ubunge kuwania jimbo la Tarime Vijijini.

‎Kumbe wapo baadhi ya viongozi wanathamini na kutambua kundi hili akiwemo Nyangwine aliyeacha alama hiyo na kumbukumbu nzuri kwa Waandishi wa Tarime hivyo ni matumaini yetu kuwa viongozi wengine wataiga mifano hii miwili mizuri kwa vitendo na si kwa maneno kwani tasnia hii ni muhimu kwenye Jamii ingawa imekuwa ni sekta yenye misukosuko na inayosahaulika kwenye kupewa hata motisha pale zinapotolewa kwenye tasnia nyingine.

Latest Posts

Don't Miss

Stay in touch

To be updated with all the latest news, offers and special announcements.

error: Content is protected !!