Latest Posts

MWANACHAMA WA YANGA “TUNA IMANI NA MAFANIKIO YA 2025 KWA TIMU YETU”

Mdau maarufu wa michezo na mwanachama wa klabu ya Yanga ameendelea kuunga mkono jitihada za Rais Samia Suluhu Hassan katika sekta ya michezo, hususan kupitia ufadhili wa goli la Mama Hussein Makubi Mwananyanzala.

Akiwatakia heri ya Mwaka Mpya 2025, mdau huyo amempongeza Rais kwa mchango wake mkubwa katika kuboresha maendeleo ya michezo nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Mwananyanzala, alisisitiza umuhimu wa kuendelea kuunga mkono jitihada za Rais Samia kwa jinsi anavyoonyesha kujitoa katika kuboresha sekta ya michezo.

“Rais wetu ameonyesha dhamira ya kweli ya kukuza michezo nchini. Hii ni hamasa kubwa kwetu wadau na mashabiki kuendelea kutoa sapoti kwa timu zetu za michezo,” alisema.

Pia, aliwatakia mafanikio makubwa wachezaji wa Yanga na wanachama wa timu hiyo pamoja na wale wa Simba kwa mwaka 2025. Alionyesha imani kubwa kuwa klabu ya Yanga itaendelea kufanya vizuri kwenye ligi mbalimbali kutokana na mipango kabambe inayotekelezwa na uongozi wa klabu hiyo.

“Hali inatupa matumaini makubwa. Nikiwa kama mwanachama wa Yanga, nina hakika tuna nafasi nzuri ya kuendelea kuvuna mafanikio kwenye mashindano mbalimbali. Kwa mwaka 2025, tunatarajia makubwa zaidi,” aliongeza.

Salamu zake za Mwaka Mpya ni ujumbe wa kutia moyo kwa viongozi wa michezo, wachezaji, na mashabiki wa Yanga na Simba huku akisisitiza mshikamano na utengenezaji wa mazingira bora ya michezo nchini.Mdau maarufu wa michezo na mwanachama wa klabu ya Yanga ameendelea kuunga mkono jitihada za Rais Samia Suluhu Hassan katika sekta ya michezo, hususan kupitia ufadhili wa goli la Mama Hussein Makubi Mwananyanzala. Akiwatakia heri ya Mwaka Mpya 2025, mdau huyo amempongeza Rais kwa mchango wake mkubwa katika kuboresha maendeleo ya michezo nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Mwananyanzala, alisisitiza umuhimu wa kuendelea kuunga mkono jitihada za Rais Samia kwa jinsi anavyoonyesha kujitoa katika kuboresha sekta ya michezo. “Rais wetu ameonyesha dhamira ya kweli ya kukuza michezo nchini. Hii ni hamasa kubwa kwetu wadau na mashabiki kuendelea kutoa sapoti kwa timu zetu za michezo,” alisema.

 

Pia, aliwatakia mafanikio makubwa wachezaji wa Yanga na wanachama wa timu hiyo pamoja na wale wa Simba kwa mwaka 2025. Alionyesha imani kubwa kuwa klabu ya Yanga itaendelea kufanya vizuri kwenye ligi mbalimbali kutokana na mipango kabambe inayotekelezwa na uongozi wa klabu hiyo.

“Hali inatupa matumaini makubwa. Nikiwa kama mwanachama wa Yanga, nina hakika tuna nafasi nzuri ya kuendelea kuvuna mafanikio kwenye mashindano mbalimbali. Kwa mwaka 2025, tunatarajia makubwa zaidi,” aliongeza.

Salamu zake za Mwaka Mpya ni ujumbe wa kutia moyo kwa viongozi wa michezo, wachezaji, na mashabiki wa Yanga na Simba huku akisisitiza mshikamano na utengenezaji wa mazingira bora ya michezo nchini.

Latest Posts

Don't Miss

Stay in touch

To be updated with all the latest news, offers and special announcements.

error: Content is protected !!