Latest Posts

KIWANDA CHA GF VEHICLES ASSEMBLERS (GFA) CHASHEREHEKEA KUTIMIZA MAGARI 4000 KILICHOTENGENEZA

Kiwanda kikubwa na cha kwanza kutengeneza na kuunganisha Magari nchini Tanzania GF vehicles Assemblers (GFA) kilichopo Kibaha mkoani Pwani kimetimiza utengenezaji wa gari ya miamoja (4000) tangu kuanza uzalishaji rasmi wa kiwanda hicho 2020.

Meneja mkuu wa kiwanda hicho ,Ezra Mereng akizungumza na wafanyakazi

Akizungumza wakati wa sherehe za kuruhusu gari ya 4000 kukanyaga ardhini baada ya kuunganishwa tayari kwa kutembea, Meneja mkuu wa kiwanda hicho, Ezra Mereng alisema wanaishukuru serikali kupendekeza Tozo ya  maendeleo ya viwanda kwenye vichwa vya Terla za magari makubwa vinavyoagizwa nchini kwa asilimia 10 ili kuvilinda viwanda vya ndani na kuchochea ununuzi wa magari yalionunganishwa nchini alimaliza manger

Mkurugenzi wa GF vehicles Assemblers (GFA), Ally Jawad Karmali akizungumza na wafanyakazi wa kiwanda hicho wakati wa sherehe za uundwaji wa gari ya 4000 iiliyotengenezwa katika kiwanda hicho na mafundi wa ndani kutoka vyuo mbalimbali nchini kwa kushirikiana na wataalamu wa kigeni iliyofanyika kibaha mkoani Pwani.

Kwa upande wa Mkurugenzi wa GFA, All Jawad Karmali amesema wao wamejipanga katika kuhakikisha wanaongeza mtaji katika uwekezaji ili kukabiliana na soko la Afrika mashariki na kati kwa upande wa magari na Tanzania kuwa nchi mojawapo inayounganisha magari na kulisha ukanda wote wa Afika mashariki na hii inatokana na mazingira mazuri ya serikali kwa wawekezaji nchini

Pia alizitaka tasisisi za serikali na kuagiza magari ambayo hayajaunganishwa na kazi ya kuunganisha ifanyike na viwanda vya ndani ili kukuza pato la taifa na kuongeza ajira kwa watanzania, pia kama nchi itajipatia fedha za kikgeni kwa kuuza nchi jirani magari yanayotoka Tanzania.

Latest Posts

Don't Miss

Stay in touch

To be updated with all the latest news, offers and special announcements.

error: Content is protected !!