Latest Posts

TAMESOT YAMLILIA NDUGAI, CHAKUMBUKA MCHANGO WAKE KWA CHAMA

Na Theophilida Felician.

 

Katibu mkuu wa chama cha waganga wa tiba asili nchini TAMESOT  Bw  Lukas Joseph  Mlipu kwa niaba ya wanachama wenzake ameelezea namna walivyopokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha spika mstaafu Job Yustino Ndugai kilichotokea  Tarehe 6 Agost 2025 jijini Dodoma.

Katibu huyo akizungumza na chombo hiki kwa njia ya simu akiwa katika mwendelezo wa ziara ya kuhamasisha  waganga kushiriki wiki ya tiba asili ya mwafrika Mbarali mkoani Mbeya amesema Marehemu Job Ndugai alikuwa ni mchango mkubwa kwa chama kwani alitoa ushauri wa karibu na wenye  kukijenga, aliwahi kuwa msaada kwa chama baada ya kukisaidia mawazo yenye kuutatua mgogoro uliokuwa ndani ya chama mwaka 2018 na kutatuliwa 2019 kipindi hicho akiwa spika wa Bunge.

Amesema kutoka na ushauri wake chama kilisimama imara na  sasa kinaendelea vizuri, hivyo  hadi  umauti unamkuta alikuwa ameishatoa ahadi ya  kuunga mkono chama kwa kutoa mchango juu ya kusaidia ujenzi wa ofisi ya chama taifa iliyojengwa mamlaka ya mji mdogo Kibaigwa Dodoma.

“Ni mambo mengi  tumeshirikiana naye hata baada ya kustaafu uspika  hususani alipokuwa akishiriki matukio ya kijamii TAMESOT tulihakikisha tunaungana naye bega kwa bega, hakika tutaendelea kumkumbuka daima aliitambua na kuithamini tiba asili kwa nguvu zote tumempoteza mtu muhimu sana” Katibu Mkuu Lukas Joseph Mlipu.

Kufuatia kifo hicho ametoa pole kwa familia, wananchi wa Kongwa na serikali kwa ujumla huku akiwasihi wanachama kuwa watulivu kipindi hiki kigumu na kuendelea kumuombea dua njema na yenye kumtakia mapumziko mema.

Latest Posts

Don't Miss

Stay in touch

To be updated with all the latest news, offers and special announcements.

error: Content is protected !!