Latest Posts

VIONGOZI WANAWAKE WA KISIASA WAJENGEWA UWEZO WA KISIASA-RUVUMA

 

Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa wanawake Tanzania (UWT) Ndg. Zainab khamis Shomar akisisitiza jambo katika Mafunzo ya Uongozi wa Kisiasa kwa Wanawake yaliyofanyika Septemba 26, 2024 wilayani Songea mkoani Ruvuma. 

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), Mary Pius Chatanda akitoa mada wakati wa Mafunzo ya Uongozi wa Kisiasa kwa viongozi wanawake yaliyofanyika Septemba 26, 2024 wilaya ya Songea mkoani Ruvuma.
Viongozi wanawake wakifuatilia mada zilizokuwa zinawasilishwa katika Mafunzo ya Uongozi wa Kisiasa kwa Viongozi Wanawake

 

 

 

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Taifa,Mary Pius Chatanda amesema kuwa katika kipindi cha miaka miwili jumuiya hiyo imekuwa ikiandaa mafunzo kwa viongozi wake kuanzia ngazi ya matawi, kata,wilaya na mikoa pamoja na watumishi wake yenye lengo la kuongeza ufanisi wa utekelezaji wa majukumu katika nyanja za kisiasa, wlimu, kiafya pamoja na mtumizi ya nishati safi.

Mwenyekiti Chatanda ameeleza hayo leo Septemba 26, 2024 wakati wa ufunguaji wa mafunzo hayo yaliyofanyika wilaya ya Songea mjini mkoani Ruvuma.

Mafunzo hayo yanafanyika kwa siku mbili yakifuatiwa na Kikao cha Baraza Kuu la UWT kitakachonyika tarehe 28 Septemba, 2024 ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Latest Posts

Don't Miss

Stay in touch

To be updated with all the latest news, offers and special announcements.

error: Content is protected !!