Latest Posts

MAAFISA POLISI WAGUSA MAISHA YA MZEE LUSAWA SUMBAWANGA

Jeshi la Polisi Mkoa wa Rukwa limeendelea kuimarisha uhusiano na jamii kwa kumtembelea na kumfikishia msaada mzee Godfrey Lusawa, mkazi wa Mtaa wa Katai, Manispaa ya Sumbawanga kutokana na maisha anayoishi.

Msaada huo umetolewa Julai 18, 2026, na maafisa wa Jeshi la Polisi wakiongozwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, SACP Shadrack Masija, baada ya Polisi Kata wa Kata ya Lwiche Mkaguzi wa Polisi Pendo Nungu kukutana na Mzee huyo wakati akitekeleza mjukumu yake ya kueneza Falsafa ya Polisi Jamii yenye malengo ya kujenga mahusiano na jamii ili kushirikiana na Jeshi la Polisi katika kubaini na kuzuia uhalifu kwani kila mmoja wetu anahitaji usalama wa maisha na mali zake.

Mzee Godfrey Lusawa amelishukuru Jeshi la Polisi kwa msaada huo, akisema umempa faraja na kumsaidia katika mahitaji muhimu ya maisha, ikiwemo chakula na sehemu salama ya kulala.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Katai, Bwana Rebi Msukwa, akizungumza kwa niaba ya wananchi, amelishukuru Jeshi la Polisi kwa hatua hiyo, akisema ni mfano wa upendo na mshikamano unaopaswa kuigwa na jamii katika kuwajali wazee.

Latest Posts

Don't Miss

Stay in touch

To be updated with all the latest news, offers and special announcements.

error: Content is protected !!