Latest Posts

WANANDEMBO WAIOMBEA AMANI TANZANIA KUELEKEA UCHAGUZI MKUU

Na Theophilida Felician, Kagera.

Umoja wa wanandembo nchini umeelezea juhudi zinazofanyika kufanya maombi wakiiombea nchi ili kufanikiwa salama zoezi muhimu la uchaguzi mkuu unaotarajia kufanyika mwezi Oktoba mwaka huu 2025.

Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa umoja huo taifa Omulangi  Domina Angribelt Abraham akiwa na baadhi ya wanaumoja baada ya kuweka kibao chenye utambulisho wa huduma zao katika mzunguko wa barabara kuu  ya Uganda road kata  Rwamishenye manispaa ya Bukoba.

Mwenyekiti Domina amesema  kuwa wao ni watu wanaotoa huduma ya maombezi kwa jamii  kupitia ibada za asili kwa sasa wamejikita kuliombea amani na utulivu taifa kama ilivyo kwa watu wengine hususani viongozi wa dini na taasisi mbalimbali zenye kuihamasisha amani.

Amefafanua  kwamba amani ni msingi wa taifa lolote duniani hivyo watanzania  hawanabudi kuungana pamoja na kuilinda kwa uchungu na   nguvu zote.

Majukumu ya wanandembo  Domina ameyataja kuwa ni pamoja na  kuhamasha jamii kuenzi na kuhifadhi mila na desturi,  kufundisha  upendo,  maadili yanayohusu familia, jamii na taifa pamoja na kuweka msukumo kwenye mafunzo ya kijamii yenye asili ya kitamaduni ambapo wamefanikiwa kuwafikia wananchi wengi wanaojitokeza maeneo yao maalumu (Murulembo) kata Kashai kupata tiba ya maombezi wakiwemo wagonjwa na wenye changamoto kadha wa kadha

Hata hivyo ameongeza kwamba wanafanya hivyo kumuunga mkono Chifu mkuu Hangaya ambaye ni Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kutokana nania yake njema ya kuunga   mkono suala la mila na desturi ambazo zimeanza kupotea kwenye jamii zetu.

Ameishukuru serikali ngazi ya taifa, mkoa na wilaya kwa namna inavyoshirikiana nao ili kuhakikisha shughuli zao zinaendelea vizuri bila  ya vikwazo.

Mwenyekiti huyo akiambatana na mwenyekiti wa umoja  huo  kwa  mkoa kagera Donatha Pangarace,  baadhi ya waamini wake na balozi wa umoja, pamoja wamesisitiza suala la kuzingatia  maadili wakifafanua kwamba kwa sasa kiwango cha maadili kimepungua kwenye jamii makundi yote watoto kwa wakubwa hali siyo nzuri.

Balozi wa wanandembo Richard Leonard Mushashu amebainisha  kuwa kushuka kwa maadili kumechangia baadhi ya  matukio  maovu ya wizi, ulevi, mauaji na mifarakano katika familia ambapo amesisitiza jamii iludi kwenye mstari na kuzingatia mila na desturi zinazosaidia kuijenga jamii iliyo bora.

Latest Posts

Don't Miss

Stay in touch

To be updated with all the latest news, offers and special announcements.

error: Content is protected !!