Latest Posts

KISA USALAMA WA RAIA, BAVICHA MBEYA WAMVAA IGP WAKITAKA UWAJIBIKAJI

Na Josea Sinkala, Mbeya.

Baraza la Vijana wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo- CHADEMA (BAVICHA) mkoa wa Mbeya, limeeleza kusikitishwa kwake na kuendelea kusikika kwa matukio ya utekaji na kupotea kwa raia hasa wanaoonekana kuwa wapinzani.

Hayo yameelezwa na Mwenyekiti wa BAVICHA Mbeya Elisha Evaristo Chonya, wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Mbeya kuhusu mambo kadhaa nchini ikiwemo tukio la kutekwa kwa katibu wa BAVICHA mkoa wa Mwanza na watu wasiofahamika.

Chonya, amelitaka Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza kuchunguza na kuwabaini wahusika wa utekaji huo huku akimtaka pia Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) kutupia jicho matukio ya utekaji na kupotea kwa wananchi, wajibu ambao pia ameutaka kwa viongozi wa mitaa, kata, wilaya na viongozi mbalimbali wakiwemo wa kisiasa.

Mwenyekiti huyo wa BAVICHA mkoa wa Mbeya, amesema wananchi wamefikia kiwango cha mwisho cha uvumilivu ambacho ni vyema kikatazamwa kwa upekee ili kuendelea kutunza amani ya nchi kwa kuhakikisha serikali na mamlaka zake zinawajibika kulinda raia na mali zao na kuhakikisha watu waliopotea katika mazingira ya kutatanisha wanapatikana.

Sanjari na kulia na utawala wa awamu ya sita kwa madai kuwa hauna utawala wa sharia, Chonya ameeleza mfumo mbovu wa ukusanyaji taka uliopo katikati mwa jiji hilo tofauti na hapo awali ambapo anasema ndio chanzo cha kulipuka kwa ugonjwa wa kipindupindu na kuitaka Halmashauri ya Jiji la Mbeya kurejesha mfumo wa maguba ili wananchi kutupa taka badala ya kukaa na taka kwenye makazi yao.

Latest Posts

Don't Miss

Stay in touch

To be updated with all the latest news, offers and special announcements.

error: Content is protected !!