Latest Posts

TPHPA YAOKOA ZAIDI YA TANI MILIONI 1.4 ZA MAZAO NA KUFUNGUA MASOKO MAPYA YA NJE.

Tanzania imefikia kiwango cha utoshelevu wa chakula cha asilimia 130, huku uzalishaji ukifikia tani 23.8 milioni katika mwaka wa fedha 2025/2026, huku Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA) ikisema hatua za kudhibiti visumbufu zimewezesha kuokoa zaidi ya tani milioni 1.4 za mazao ya nafaka.

Takwimu hizo zimetolewa leo Agosti 27, 2026, na Mkurugenzi Mkuu wa TPHPA, Prof. Joseph C. Ndunguru, akieleza mafanikio ya Mamlaka kwa mwaka wa fedha 2025/2026 na mipango ya mwaka 2026/2027.

Kwa mujibu wa Ndunguru, TPHPA imedhibiti kwelea kwelea milioni 233.5 katika wilaya 21, hatua iliyosaidia kuokoa takribani tani 1,092,780 za nafaka ambapo udhibiti wa viwavijeshi katika Halmashauri 52 uliwezesha kuokoa takribani tani 342,787.5 za mazao baada ya kutumika lita 54,846 za viuatilifu katika mashamba yenye ukubwa wa ekari 228,525.

Kwa upande wa masoko ya kimataifa, TPHPA imewezesha kampuni nane mpya za Tanzania kuanza kusafirisha parachichi kwenda China, na kufanya jumla ya kampuni zilizoruhusiwa kufikisha zao hilo katika soko hilo kufikia 24.

Pia, kampuni 444 za Tanzania zimesajiliwa katika mfumo wa forodha wa China (GACC) kwa ajili ya kusafirisha mazao mbalimbali.

Amesema Mamlaka hiyo pia imefungua masoko mapya kwa mazao ya Tanzania, yakiwemo parachichi kwenda Afrika Kusini, India na China, soya kwenda China, mashudu ya pamba na alizeti kwenda China, mahindi ya njano kwenda Misri, ndizi mbichi kwenda Afrika Kusini na mazao mbalimbali kwenda Seychelles.

 

” Hadi Juni 2026, soko la Seychelles lilikuwa limefunguliwa kwa mazao 10, yakiwemo kabichi, parachichi, maharage mabichi, karoti, viazi, tangawizi na nanasi,TPHPA imeendelea pia kulinda masoko yaliyopo,”ameeleza

Latest Posts

Don't Miss

Stay in touch

To be updated with all the latest news, offers and special announcements.

error: Content is protected !!