Latest Posts

WAHANDISI WASHAURI WATAKIWA KUSIMAMIA KWA UKARIBU UJENZI WA MIUNDOMBINU YA BARABARA

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) -Miundombinu Mhandisi Rogatus Mativila amewataka Wahandisi washauri wanaosimamia miradi mbalimbali ya miundombinu ya Barabara nchini kusimamia kwa ukaribu miradi hiyo ili ikamilike kwa wakati.

Mhandisi Mativila ameyasema hayo tarehe 10 Juni, 2024 wakati akikagua ujenzi wa jengo la ofisi la Wahandisi katika Manispaa ya Tabora ambalo lipo chini ya mradi wa TACTIC unaosimamiwa na TARURA.

“Mheshimiwa Rais Dkt. samia Suluhu Hassan anahangaika kutafuta fedha ili kuhakikisha wananchi wanapata Barabara, wataalam lazima mbadilike na kusimamia kwa ukaribu ujenzi wa miradi hii, Mkandarasi huyu angekuwa anasimamiwa kwa ukaribu angeshakuwa amemaliza hapa” -Mhandisi Mativila.

Hata hivyo Mhandisi Mativila amewataka wataalam hao kuhakikisha wanasimamia ubora wa ujenzi ili wakandarasi wakamilishe kazi kwa wakati.

Aidha, amemtaka Mhandisi Mshauri UNITEC Civil Consultants Ltd kuhakikisha anasimamia kwa karibu ujenzi huo na ifikapo mwezi Agosti mwaka huu jengo hilo liwe limekamilika.

Ujenzi wa jengo la ofisi la Wahandisi linalogharimu takriban milioni 800 lilianza ujenzi wake Novemba 2023 na lilitarajiwa kukamilika 15 Juni, 2024, ambapo sasa ameagiza ujenzi huo uwe umekamilika ifikapo Agosti 2024, jengo hilo linajengwa na Mkandarasi CICO Contractor.

Latest Posts

Don't Miss

Stay in touch

To be updated with all the latest news, offers and special announcements.

error: Content is protected !!